Kukata Tamaa Quotes

We've searched our database for all the quotes and captions related to Kukata Tamaa. Here they are! All 5 of them:

Kitu kikishindikana katika maisha yako kamwe usikate tamaa kwa sababu kushindwa ni mama wa mafanikio na kukata tamaa ni mama wa kushindwa.
Enock Maregesi
Musa alipokuwa mlimani kupokea Amri Kumi za Mungu kwa ajili ya Wana wa Israeli alikawia sana kurudi, kiasi cha watu kukata tamaa na kujiona wapweke wakiwa njiani kuelekea katika Nchi ya Ahadi. Kutokana na woga usio na kifani na kukata huko kwa tamaa waliamua kutosubiri tena kusikia neno kutoka kwa Mungu, au kuiona sura halisi ya Mungu kama Musa alivyokuwa amewaahidi, hivyo wakamlazimisha Haruni awatengenezee mungu kutokana na taswira ambayo tayari walishakuwa nayo vichwani mwao kuhusu mungu waliyemtaka; yaani ndama wa dhahabu, au mungu mpya ambaye angewapa chochote walichotaka muda wowote waliotaka.
Enock Maregesi
Mawazo ya kukata tamaa yanaweza kusababisha tukamtengeneza au kumbuni tena Mungu kwa mfano wetu sisi wenyewe, mfano ambao kwa kawaida ni tofauti kabisa na mfano unaozungumzwa ndani ya Biblia. Hivyo tunaishia kutumikia mfano badala ya kumtumikia Mungu wa kweli.
Enock Maregesi
Kila binadamu ana nguvu ya ziada katika mwili wake ijulikanayo kitaalamu kama ATP. ATP (‘Adenosine Triphosphate’) ni molekuli ndogo zaidi iliyoko ndani ya seli ambayo kazi yake ni kutengeneza nguvu ya ziada kwa ajili ya seli, na kwa ajili ya mwili mzima kwa jumla, pale mwili unapoonekana kukata tamaa au kuishiwa na nguvu kabisa. Ni kama jenereta ya umeme kwa ajili ya seli, inayofanya kazi pale umeme wa kawaida unapokatika.
Enock Maregesi
Kuamsha ATP lazima kwanza ukate tamaa. Lazima kwanza uishiwe na nguvu. Kisha ujilazimishe, au ulazimishwe na mazingira, kufanya jambo.
Enock Maregesi