Hekima Quotes

We've searched our database for all the quotes and captions related to Hekima. Here they are! All 43 of them:

β€œ
Hekima ni ufunguo wa kufanya maamuzi mema kulingana na msingi wa maarifa ya Biblia.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Kuna tofauti kati ya hekima na maarifa. Unaweza kuwa profesa ukawa mpumbavu, unaweza kuwa gumbaru ukawa na hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Kupata maarifa kutokana na shida ni jambo la kawaida maana shida ni kipimo cha akili, lakini kupata maarifa bila shida ni hekima maana hekima ni ufunguo wa maamuzi mema na udadisi wa kiakili.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Ukarimu ni bora kuliko hekima, na kulitambua hilo ndiyo mwanzo wa hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Hekima ni fikra inayotoka moyoni, busara ni hekima inayozungumzwa.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Kupata maarifa kutokana na shida ni jambo la kawaida, lakini kupata maarifa bila shida ni hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Neno moja kutoka mdomoni mwako linaweza kukuletea madhara makubwa. Fikiria kwanza maana ya kitu unachofikiria (ambacho tayari umekisema kichwani mwako) kabla ya kukisema tena mdomoni mwako. Wenye hekima huzungumza kwa sababu wana kitu cha kuzungumza. Wapumbavu hubwabwaja.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Mungu ni mwingi wa hekima, lakini kwa nini alimuumba Shetani? Kwa sababu, Shetani wakati mwingine ni hekima. Ukiendelea kupigwa, bila wewe kupiga, unaweza kuumia, familia yako inaweza kuumia pia! Kuepusha matatizo ya familia yako, wakati mwingine unahitaji kupigana.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Geuza hasira yako kuwa hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Heshima hujengwa kwa hekima, haijengwi kwa misuli.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Utajiri wa nje huwa unaanzia ndani, nao ni hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Mungu hagawi pesa kwa watu kama watu wanavyofikiria. Anagawa upendo na hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
kuwajua wengine ni hekima, kujijua mwenyewe ni maarifa makubwa
”
”
Lao Tzu
β€œ
Ukitaka watu wakuheshimu usitumie mabavu. Tumia hekima. Maana, watu hawaheshimu wewe ni nani au unatoka wapi, wanaheshimu nguvu ya matendo yako. Kama una tatizo na mtu usichukue uamuzi wa haraka. Ongea na watu kupata hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Maisha tunayoishi ni mafupi, maisha ya mbinguni ni ya milele. Fundisha familia yako upendo na hofu ya Mungu, kwani hiyo ndiyo akili kushinda zote. Hekima ya kutunza familia inapatikana katika kitabu cha Mithali cha Agano la Kale.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Hasanati ni matendo mema. Mema yanatoka kwa Mungu. Mabaya yanatoka kwa Shetani. Mke mwema anatoka kwa Mungu. Mke mbaya anatoka kwa Shetani. Mke mwema ana hekima na busara, ana maadili na tabia njema, ana utu na uchapakazi, ana wema na upendo, na ana aibu kwa wanaume.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Hasira ni Shetani. Hekima ni Mungu. Kila kitu kimo ndani yetu. Hasira imo ndani yetu. Hekima imo ndani yetu. Atomu ni matofali ya ujenzi wa kila kitu ulimwenguni likiwemo jua na miili ya wanadamu. Ndani ya atomu kuna nguvu ya chanya na kuna nguvu ya hasi. Kama miili yetu imetengenezwa na atomu na katika kila atomu kuna nguvu ya chanya na kuna nguvu ya hasi, hivyo basi, tuna uwezo mkubwa wa kufanya mambo mazuri na tuna uwezo mkubwa wa kufanya mambo mabaya. Mtu akikutukana mwambie asante. Akikupiga mwambie asante. Akiendelea kukupiga, pigana. Geuza hasira yako kuwa hekima kwa faida yako na kwa faida ya wengine.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Ikiwa huna pesa na una mke na watoto kwa mfano, mke wako (wanawake walio wengi) hatakuona wa maana kwa sababu ya ustawi wa maisha ya familia yake. Ikiwa una mwanamke asiyekuwa na busara au hekima ya kutosha, au mwanamke ambaye akili zake zimefyatuka kidogo, atakusaliti kutafuta bwana au mtu mwenye maana. Kama huna pesa huna maana kwa mwanamke.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Kinachotokea katika dunia hii si kitu kizuri cha kuzoea au hata kufikiria. Hivyo tuna haki ya kuwa na mawazo, hasira na wanyonge kuhusiana na suala zima la maisha yetu hapa duniani. Hata hivyo hali hii itabaki kuwa hivyo kwa sababu Mungu ametaka iwe hivyo kwa sasa. Kwa maana hiyo, hekima ni kukubaliana na mapenzi ya Mungu. Lazima tukubaliane na kisichoweza kufikirika kuweza kubadilika.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Palestina ni nchi ya Waisraeli waliyopewa na Mungu wa Yakobo. Hata hivyo, hawakutimiza masharti. Mungu aliwaagiza kuua kila mtu katika nchi ya Kaanani na miji yake yote. Waisraeli, wakiongozwa na Yoshua, waliua watu wengi katika nchi ya Kaanani. Hawakuua kila mtu katika miji ya Ashdodi, Gathi na Ukanda wa Gaza kama walivyoagizwa. Mungu alimwambia Ibrahimu kuwa angempa yeye na uzao wake nchi ya Kaanani kuwa milki yao ya milele, na kuwa Yeye ndiye angekuwa Mungu wao daima. Vita ya Israeli na Palestina itamalizwa na Mungu. Itamalizwa na hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Simama nyuma ya maneno uliyoyasema mara mbili: kichwani na mdomoni mwako. Simama nyuma ya maneno uliyoyasema kwa hekima. Usiyumbe hata mambo yatakapokwenda segemnege.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Maarifa unayoyatafuta katika Biblia, Kurani au Yoga ('Oriental Yoga': 'esoteric knowledge': maarifa ya kujua siri ya uumbaji wa Mungu ya 'Kabbalah' ya Kiyahudi au 'Kalachakra' ya Kibudha ya bara la Asia; siri ya sayansi ya kurefusha maisha ya mafundisho ya kiroho ya 'Arcanum' ya Misri – au Kemia ya Mungu au 'Alchemy'; mafundisho ya kiroho ya 'Rosicrucia' ya bara la Ulaya tangu mwishoni mwa karne ya kumi na nne; 'sex magic', 'sex magic' inaweza kukupa utajiri au umaskini hivyo kuwa makini; n.k.) ni hekima na busara. Vingine vyote vitajileta vyenyewe.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Aidha, tunaweza kupata inkishafi kutokana na asili ya miili yetu, matukio fulani ya wakati ujao yana asili yake katika ndoto za binadamu. Ndoto hizo au maono hayo ni ishara ya kile kinachokuja mbele katika maisha ya mtu; kama vile afya, ugonjwa au hatari. Ukiota kuhusu moto, hiyo ni ishara ya hasira – unatakiwa kuwa na hekima; ukiota kuhusu mimba na unajifungua, hiyo ni ishara ya kuwa katika mchakato wa kutengeneza wazo jipya – unatakiwa kushukuru; ukiota unaruka angani, hiyo ni ishara ya tumaini – unatakiwa kushukuru; ukiota kuhusu maji au kiowevu kingine chochote kile, hiyo ni ishara ya siri na wakati mwingine ni ishara ya kuwa na matatizo ya kiafya kama utaota kuhusu maji machafu – unatakiwa kuwa msiri na msafi; ukiota kuhusu ardhi, hiyo ni ishara ya huzuni – unatakiwa kuomba; na ukiota kuhusu Yesu, hiyo ni ishara ya mafanikio – unatakiwa kushukuru.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Some write because they love to, some write because they have talent…, I write because I have something to say…, and I think that something has yet to be said just the way I want it to be said…
”
”
Busara Bin Hekima
β€œ
Leo ni siku ya kumbukumbu ya giza lililoingia katika familia ya Enock Maregesi. Tarehe 4/11/14 ni siku nuru ya mwanga wa maisha ya nyanya yangu mpenzi Bi Martha Maregesi ilipozimika huko Musoma. Leo ni miaka miwili ametimiza akiwa kimya kabisa! Sikisikii tena kicheko chake wala siisikii tena hekima yake! Familia yake inamkumbuka sana. Palipokuwa kwake ni nyumbani kwetu. Hatuwezi kusahau upendo wake na umuhimu wake kwetu. Tulimpenda sana, lakini Mungu wa mbinguni alimpenda zaidi.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Mfalme Sulemani alikuwa mtu mwenye hekima kuliko wote ulimwenguni. Anatushauri, β€œAdui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na BWANA atakupa thawabu (Mithali 25:21-22). Yesu anasema jambo fulani linalofanana sana na hilo katika mafundisho Yake yaliyofuata (Mathayo 5:44-45). Kitendo cha kutukanwa, kupigwa, kushtakiwa au kulazimishwa kubeba mzigo mzito usio wa kwako kinaweza kusababisha mafutu mabaya kabisa katika asili ya binadamu. Yaani, chuki, hasira, ukatili na hata vurugu. Lakini pale wale waliobarikiwa kuwa na hekima wanapojikuta katika majaribu makubwa kama hayo tabia yao haitakiwi kuwa ya shari, inda au ya kulipiza kisasi. Bali inatakiwa kuwa ya kusaidia, kuwa na ridhaa ya kutenda mambo mema, na kuwa mwema kwa wengine siku zote.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa raha ni rahisi kuliko kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa shida, na utahitaji imani kuendelea kumwamini wakati wa dhiki. Vipindi vigumu katika maisha yetu hutokea kwa kila mmoja wetu. Kuamini ya kwamba Mungu ana makusudi ya lazima kukuondolea vikwazo katika maisha yako ni vigumu sana wakati mwingine, lakini imani ndicho kitu cha muhimu zaidi unachotakiwa kuwa nacho katika kipindi hiki ambacho dunia imekata tamaa. Amani ya Mungu, ambayo huzidi hekima na maarifa yote ya kibinadamu, ni kuliamini neno la Mungu kwamba ni la kweli. Bila imani hutaweza kumfurahisha Mungu. Imani ni ufunguo wa nguvu, uwezo na neema ambavyo Mungu ametupangia. Kwa ufupi, Mungu ni mkubwa kuliko wewe na matatizo yako.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Mungu hatakubali kuwa na mtu katika ufalme wake ambaye hatakubali kutawaliwa naye. Usikubali kutawaliwa na Ibilisi, kubali kutawaliwa na Mungu. Ni jukumu letu kuanza kuishi sasa kama vile tutakavyoishi mbinguni. Shetani anataka uwe na hekima ya duniani ili akupumbaze. Lakini hofu ya Mungu ndiyo msingi wa hekima ya kweli. Ukitaka asikupumbaze, pokea Roho ya Mungu kwa kubatizwa. Ukiipokea Roho ya Mungu utajua mambo ya Mungu, ambayo dunia haiwezi kujua.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Matatizo ya kijamii, kimiiko, kimaadili, kisiasa, na kiroho; hayataweza kutatuliwa kwa pesa, vikao vya kifamilia, haki za binadamu, usalama wa taifa, au nguvu za kijeshi. Yataweza kutatuliwa kwa haki na hekima ya Mwenyezi Mungu.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Israeli ilifikia kikomo cha kipindi chake kikubwa cha mafanikio tangu enzi za Sulemani. Taifa lilikuwa tajiri. Lilikuwa na nguvu. Lilikuwa na silaha nyingi na nzuri zaidi. Lilikuwa taifa lililojidai kwa uwezo wake mkubwa wa nguvu za kijeshi, hekima, ujasiri, utajiri, na faida za kimkakati. Nani angeweza kushindana na Israeli? Lakini Mungu hunguruma onyo kwamba uwezo wote mkubwa wa asili wa taifa, ujuzi waliojipatia, na sifa bora zaidi havikuweza kulisaidia taifa la Israeli. Watu huona nguvu ya taifa katika utajiri wake, idadi yake ya watu, silaha za kijeshi, teknolojia, na maarifa. Lakini Mungu huangalia haki.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Si vizuri kuonyesha moyo wa upendo kwa wanao, kwani hiyo ni hekima ya kukataliwa, isipokuwa kwa wengine.
”
”
Simon Mashalla
β€œ
Kuna siku mbili tu za muhimu zaidi katika maisha yako kama alivyosema Mark Twain: Siku uliyozaliwa na siku uliyojua kwa nini ulizaliwa. Siku utakapojua kwa nini ulizaliwa utakuwa tajiri, wa mali na hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Siku moja, jambo baya litatokea. Labda babu yako au mnyama wako kipenzi atafariki au shangazi yako atagundulika na kansa. Labda utafukuzwa kazi au utaachika kwa mumeo au mkeo mliyependana sana. Labda rafiki yako kipenzi atapata ajali mbaya ya gari na utatakiwa kupeleka taarifa kwa ndugu na marafiki zake. Kutoa taarifa ya jambo baya kwa mtu ni kazi ngumu sawa na kupokea taarifa ya jambo baya kutoka kwa mtu. Kama umeteuliwa kupeleka taarifa ya kifo au ya jambo lolote baya kwa mtu fanya hivyo kwa makini. Toa taarifa ya msiba au ya jambo lolote baya kwa hekima na busara kama Ibrahimu alivyofanya kwa Sara kuhusiana na kafara ya Isaka, si kama Mbenyamini alivyofanya kwa Eli kuhusiana na kutwaliwa kwa sanduku la agano na kuuwawa kwa watoto wake wawili. Jidhibiti kwanza wewe mwenyewe kama umeteuliwa kupeleka taarifa ya kifo au ya jambo lolote baya. Angalia kama wewe ni mtu sahihi wa kupeleka taarifa hiyo. Pangilia mawazo ya kile unachotaka kwenda kukisema au unachotaka kwenda kukiandika. Mwangalie machoni, si usoni, yule unayempelekea taarifa kisha mwambie kwa sauti ya upole nini kimetokea.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Hakimu na Kuhani Mkuu wa Shilo Eli alipata matatizo makubwa wakati wa mgogoro wa Waisraeli na Wafilisti, kati ya mwaka 2871 na 2870 Kabla ya Kristo. Mara tu baada ya kupewa taarifa ya kifo cha watoto wake wawili, Hofni na Finehasi, na kutwaliwa kwa Sanduku la Agano la Bwana wa Majeshi lililohifadhi Amri Kumi za Mungu, Eli alianguka kutoka katika kiti chake na kufariki papo hapo akiwa na umri wa miaka 98. Aidha, mkwe wa Eli, mke wa Finehasi, alijifungua ghafla na kufariki alipopata taarifa ya kifo cha mkwewe na taarifa ya kuuwawa kwa mumewe na ya kutekwa nyara kwa Sanduku la Agano. Mwanajeshi kutoka Benyamini falaula angetumia hekima na busara kutoa taarifa ya kifo na ya kutwaliwa kwa Sanduku la Agano huenda Eli asingefariki, na huenda mkwewe asingejifungua mtoto njiti na huenda asingekufa siku hiyo. Kwani Sanduku la Agano lilirejeshwa nchini Israeli, na Wafilisti wenyewe, baada ya miezi saba tangu litwaliwe, na kifo cha watoto wa Eli yalikuwa mapenzi ya Mungu. Hivyo Eli asingeweza kuzuia kifo cha watoto wake, na Wafilisti wasingeweza kukaa na Sanduku la Agano milele. Lakini katika kafara ya Isaka ambapo Isaka aliamua kujitoa kafara mwenyewe kumfurahisha Mungu na baba yake kama Yesu alivyoamua kujitoa kafara mwenyewe kumfurahisha Mungu na baba yake wa mbinguni, Sara angekufa kama Ibrahimu hangetumia hekima alipomwambia anakwenda kumtolea Bwana kafara ya mwanakondoo wakati akijua anakwenda kumtoa Isaka mtoto wa pekee wa Sara. Hekima inatoka moyoni, busara inatoka mdomoni. Kwa vile suala la kutoa taarifa mbaya kwa mtu ni gumu kwa yule anayetoa na kwa yule anayepokea, hekima na busara havina budi kutumika.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Mwenye hekima huzungumza kilicho na maana! Kinaweza kuwa kizuri au kibaya.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Ni vizuri kujua mambo. Lakini ujue kwa hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Tukiacha Siasa Zinazotutawala Ziingilie Dirishani, Hekima Zinazotutawala Pia Zitatutokea Mlangoni
”
”
Wilson M Mukama
β€œ
Tanzania ina majanga mawili kuhusiana na UVIKO-19: Janga la Korona na janga la watu wasiotaka kuchanjwa! Nisikilize! Kataa kwa hekima! Acha Mungu achanjwe kwa niaba yako!
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Tujikumbushe *Wazee wanasema ni vizuri tucheke kidogo. Ng'ombe akiwa na birthday naomba kondoo wote mlete maua. Simba akikukimbiza ukikutana na pundamlia(zebra) ukirukia mgongoni simba atasimama kama gari?Kama hujawahi kuonja ladha ya sabuni muoshe mbwa. Najiwazia tuu hapa hata sina point, ukimpa fundi cherehani ashone dera la nyangumi!! Hivi kati ya hawa nani anachukia mwanga? Mwizi, kahaba na popo? Ee Mungu naomba unipe bunduki lakini nisiitumie*Wewe endelea kujifanya serious udhani kuna mtu atakusifia una hekima! Cheka ndugu yangu
”
”
©️Pd. PK!
β€œ
Mtu anaweza kuchanganyikiwa lakini akasema kitu cha hekima, akiongozwa na Roho Mtakatifu.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Iwapo watu watakwenda nje ya kusudi la Mungu, hata wawe makini kiasi gani na injili, maneno yao hata yawe ya hekima kiasi gani hayatawasaidia chochote.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Geuza kiburi chako kuwa hekima.
”
”
Enock Maregesi
β€œ
Bila kiburi hutamshinda Shetani, lakini kiburi dhidi ya Shetani unakishinda kwa hekima.
”
”
Enock Maregesi